dcsimg

Reptilia ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Reptilia (kutoka Kilatini "reptilis" mwenye kutambaa; pia: mtambaazi, mtambaachi, mnyama mtambaaji[1]) ni kundi la wanyama wenye damu baridi, ngozi ya magamba badala ya nywele au manyoya wakipumua kwa mapafu. Siku hizi wataalamu hupendelea jina Sauropsida.

Wanazaa kwa njia ya mayai; wengine wanatega mayai na wadogo wanatoka nje bila ngazi ya kiluwiluwi au kwa spishi kadhaa mayai yanaiva ndani ya tumbo la mama na wadogo wanazaliwa hai.

Kibiolojia ni ngeli ya vertebrata. Jina limetokana na maumbile yao maana wanatambaa na tumbo juu ya ardhi; ama kwa miguu mifupi kama mijusi au bila miguu kama nyoka.

Mwainisho

  • Ngeli Reptilia (au Kladi Sauropsida)
    • Kladi Eureptilia
      • Kladi Romeriida
        • Nusungeli Anapsida
        • Nusungeli Diapsida
          • Ngeli ya chini Archosauromorpha

              • Oda Saurischia
                • Nusuoda Theropoda
            • Oda ya juu Crocodylomorpha
          • Ngeli ya chini Lepidosauromorpha

Dinosauria wa kale walikuwa reptilia wakubwa sana walikwisha miaka milioni 65 iliyopita. Kufuatana na vumbuzi za hivi karibuni ndege hufikiriwa kuwa na nasaba na dinosauri (kutoka kwa nusuoda ya Theropoda).

Maelezo

  1. KAST:reptile=reptilia;KKK/ESD: reptile-mtambaazi; KKK/SED: mtambaachi-reptile,snake; KKS: mtambaachi-nyoka

Picha

Crystal Clear app babelfish vector.svg Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Reptilia kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Reptilia: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Reptilia (kutoka Kilatini "reptilis" mwenye kutambaa; pia: mtambaazi, mtambaachi, mnyama mtambaaji) ni kundi la wanyama wenye damu baridi, ngozi ya magamba badala ya nywele au manyoya wakipumua kwa mapafu. Siku hizi wataalamu hupendelea jina Sauropsida.

Wanazaa kwa njia ya mayai; wengine wanatega mayai na wadogo wanatoka nje bila ngazi ya kiluwiluwi au kwa spishi kadhaa mayai yanaiva ndani ya tumbo la mama na wadogo wanazaliwa hai.

Kibiolojia ni ngeli ya vertebrata. Jina limetokana na maumbile yao maana wanatambaa na tumbo juu ya ardhi; ama kwa miguu mifupi kama mijusi au bila miguu kama nyoka.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri