dcsimg

Chawa ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Chawa ni wadudu wadogo wa oda Phthiraptera katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa), lakini hata kama wahenga wao walikuwa na mabawa, chawa hawanayo. Wadudu hawa wote ni vidusia wa nje juu ya ndege na mamalia isipokuwa Monotremata (kinyamadege na mhanganungu), popo, nyangumi, pomboo na kakakuona. Kuna aina mbili za chawa: wanaokula nywele, manyoya na seli za ngozi zilizokufa, na wanaofyunza damu ya mwenyeji. Chawa wa aina ya kwanza wana vipande vya mdomo vya kutafuna, wale wengine wana mdomo wa kufyunza. Miguu inabeba aina za magando madogo ili kushika nywele au manyoya ya mwenyeji. Kwa kawaida mayai ya chawa yamegandia nywele au manyoya, au pengine yamewekwa ndani ya shina la unyoya.

Uharibifu wa chawa na jinsi ya kumuangamiza

Chawa wanaopatikana kichwani hawana magonjwa yoyote wanayosababisha lakini waliye mwilini huwa wanasababisha magonjwa. Hata hivyo, katika jamii nyingi, chawa huonekana kana kwamba huwasumbua walio wachafu ama wanaoishi kwa uchafu. Pia hufanya mtu adhoofike kwa sababu ya kunyonywa na vidusia hawa.

Kuna dawa kadhaa za kupuliza ili kuwaua wadudu hawa. Usafi pia ni muhimu kama wataka kuwakwepa.

Picha

Viungo vya nje

Blue morpho butterfly.jpg Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chawa kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Chawa: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Chawa ni wadudu wadogo wa oda Phthiraptera katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa), lakini hata kama wahenga wao walikuwa na mabawa, chawa hawanayo. Wadudu hawa wote ni vidusia wa nje juu ya ndege na mamalia isipokuwa Monotremata (kinyamadege na mhanganungu), popo, nyangumi, pomboo na kakakuona. Kuna aina mbili za chawa: wanaokula nywele, manyoya na seli za ngozi zilizokufa, na wanaofyunza damu ya mwenyeji. Chawa wa aina ya kwanza wana vipande vya mdomo vya kutafuna, wale wengine wana mdomo wa kufyunza. Miguu inabeba aina za magando madogo ili kushika nywele au manyoya ya mwenyeji. Kwa kawaida mayai ya chawa yamegandia nywele au manyoya, au pengine yamewekwa ndani ya shina la unyoya.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri