Tongo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Estrildidae ambao wanatokea Afrika na Asia. Wanafanana na mishigi lakini rangi zao ni nyeusi, kijivu, kahawia na nyeupe tu.
Hula mbegu hasa, lakini wadudu pia, hususa makinda.
Tago lao ni tufe la manyasi lenye mwingilio kwa kando. Jike huyataga mayai 2-7.
Tongo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Estrildidae ambao wanatokea Afrika na Asia. Wanafanana na mishigi lakini rangi zao ni nyeusi, kijivu, kahawia na nyeupe tu.
Hula mbegu hasa, lakini wadudu pia, hususa makinda.
Tago lao ni tufe la manyasi lenye mwingilio kwa kando. Jike huyataga mayai 2-7.