Kwa kipimo chenye jina la karibu angalia hapa shubiri
Mshubiri au msubili ni jina la mimea ya jenasi Aloe katika nusufamilia Asphodeloideae ya familia Xanthorrhoeaceae ambayo ni aina za sukulenti. Watu wengi wanaendelea kuweka Aloe ndani ya familia yake Aloaceae. Spishi kadhaa ni miti, lakini siku hizi huainishwa katika jenasi Aloidendron.
Majani ya mishubiri na dawa zilizotengenezwa kutoka haya huitwa shubiri.
Mimea hii ina shina fupi au haina shina kabisa, isipokuwa spishi zilizo miti. Majani ni marefu na manono na yanatoka shina karibu na wenziwe; yana miiba kingoni mwao. Maua yana umbo wa mrija mfupi na rangi yake ni nyekundu, pinki, ya machungwa, njano au nyeupe. Yapo mwishoni mwa kikonyo chenye vitawi au bila vitawi. Utomvu utokao mwenye majani hutumika kutengeneza dawa.
Spishi moja inajulikana sana: mshubirimani (Aloe vera), ambao unapandwa sana duniani na hutumika kwa kutengeneza dawa za uganga au za mitishamba.
Spishi nyingine inayopandwa sana katika Afrika na nchi nyingine za Tropiki ni mshubiri mwekundu (A. ferox).
Kwa kipimo chenye jina la karibu angalia hapa shubiri
Mshubiri au msubili ni jina la mimea ya jenasi Aloe katika nusufamilia Asphodeloideae ya familia Xanthorrhoeaceae ambayo ni aina za sukulenti. Watu wengi wanaendelea kuweka Aloe ndani ya familia yake Aloaceae. Spishi kadhaa ni miti, lakini siku hizi huainishwa katika jenasi Aloidendron.
Majani ya mishubiri na dawa zilizotengenezwa kutoka haya huitwa shubiri.
Mimea hii ina shina fupi au haina shina kabisa, isipokuwa spishi zilizo miti. Majani ni marefu na manono na yanatoka shina karibu na wenziwe; yana miiba kingoni mwao. Maua yana umbo wa mrija mfupi na rangi yake ni nyekundu, pinki, ya machungwa, njano au nyeupe. Yapo mwishoni mwa kikonyo chenye vitawi au bila vitawi. Utomvu utokao mwenye majani hutumika kutengeneza dawa.
Spishi moja inajulikana sana: mshubirimani (Aloe vera), ambao unapandwa sana duniani na hutumika kwa kutengeneza dawa za uganga au za mitishamba.
Spishi nyingine inayopandwa sana katika Afrika na nchi nyingine za Tropiki ni mshubiri mwekundu (A. ferox).