Kindi-jua ni wanyama wadogo wa jenasi Heliosciurus katika kabila Protoxerini la familia Sciuridae. Mkia yao una miviringo myeusi na kahawia au kijivu. Kama kindi wote spishi hizi hupitisha takriban saa zote mitini na huteremka nadra ardhini. Hupatikana mara nyingi wakipumzika juani, sababu ya jina lao. Wanatokea misitu ya Afrika ya Magharibi, ya Kati na ya Mashariki kutoka Senegali mpaka Eritrea na Zimbabwe. Hula mbegu, makokwa, matunda, matumba, machipukizi, wadudu, mayai na mijusi, ndege na wanyama wadogo.
Kindi-jua ni wanyama wadogo wa jenasi Heliosciurus katika kabila Protoxerini la familia Sciuridae. Mkia yao una miviringo myeusi na kahawia au kijivu. Kama kindi wote spishi hizi hupitisha takriban saa zote mitini na huteremka nadra ardhini. Hupatikana mara nyingi wakipumzika juani, sababu ya jina lao. Wanatokea misitu ya Afrika ya Magharibi, ya Kati na ya Mashariki kutoka Senegali mpaka Eritrea na Zimbabwe. Hula mbegu, makokwa, matunda, matumba, machipukizi, wadudu, mayai na mijusi, ndege na wanyama wadogo.